Vikosi vya usalama nchini Nigeria vimewaokoa wafanyakazi watano wa mashirika ya kimatatifa ya misaada waliotekwa nyara mwezi uliopita na wapiganaji wa kundi la Boko Haram katika barabara ya Monguno-Maiduguri, mkoa wa Borno, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Msemaji wa jeshi la polisi la nchi hiyo Peter Afunaya ameliambia Shirika la Habari la China Xinhua kuwa, operesheni hiyo ya uokoaji ilifanywa kwa ushirikiano na wadau wengine muhimu katika jeshi na idara ya upelelezi, na kwamba wafanyakazi hao wako katika afya nzuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |