Kiungo wa kimataifa wa Kenya, Anthony Agay Akumu amekamilisha uhamisho wa kujiunga na miamba ya soka nchini Afrika Kusini, Kaizer Chiefs akitokea Zesco United ya Zambia. Akumu ambaye pia ni mmoja wa nyota watatu wa Kenya waliokuwa katika kikosi cha mabingwa hao wa Zambia, ameondoka Zesco baada ya kumaliza mkataba wake. Akumu ameichezea timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars mara 38.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |