Mshambuliaji tegemeo wa Manchester United Marcus Rashford huenda akakosa kucheza mechi ya Ligi Kuu England itakayochezwa Jumapili kati ya timu hiyo na Liverpool baada ya kuumia katika mchezo wa kombe la FA dhidi ya Wolvehampton Wanderes. Rashford alitolewa dakika 30 baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Jesse Lingard katika mchezo huo ambao Man United ilishinda kwa bao 1 – 0 katika uwanja wao wa nyumbani Old Trafford.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |