Mchezaji wa timu ya Tottenham Hotspur ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Kenya Victor Wanyama amempongeza Anthony 'Teddy' Akumu baada ya mchezaji huyo kusaini mkataba wa miaka mitatu na timu ya Kaizer Chirsf ya Afrika Kusini. Akumu amejiunga na orodha ya wachezaji wa kimataifa wa Kenya waliocheza kwenye Ligi Kuu ya Afrika Kusini, akiwemo Musa Otieno Santos kati ya mwaka 1997 na 2011 na kushinda kombe hilo. Wengine ni Brian Mandela, Ali Abondo na Clifton Miheso.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |