Mshauri mkuu wa serikali ya Myanmar, Aung San Suu Kyi amekutana na Rais Xi Jinping wa China ambaye yuko ziarani nchini humo.
Viongozi hao wamekutana baada ya rais Xi kushiriki kwenye dhifa ya taifa iliyoandaliwa rais Win Myint wa nchi hiyo kwa ajili yake Ikulu nchini humo.
Viongozi hao wamekubaliana kufanya mazungumzo rasmi kesho, ili kubadilishana maoni kuhusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili na masuala yanayoyafuatiliwa nazo kwa pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |