Naibu waziri wa nishati wa Tanzania Subira Mgalu amesema nchi hiyo inapanga kusambaza gesi asilia katika maeneo matano yakiwemo Arusha, Dodoma, Tanga, Kilimanjaro na Morogoro kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na viwandani, ili kupunguza utegemezi kwa umeme. Shirika la Maendeleo ya Petroli la Tanzania TPDC litashughulikia ujenzi wa miundo mbinu kwa ajili ya mradi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |