Shirika la habari la serikali ya Sudan SUNA limeripoti kuwa, majeshi ya pamoja ya Sudan na Libya yamerejesha wahamiaji haramu 107 ambao waligunduliwa katika sehemu ya jangwa, Jimbo la Kaskazini nchini Sudan linalopakana na Libya. Kamanda wa majeshi hayo Jimbo la Kaskazini Jenerali Anwar Abdalla Nagodi amesema wahamiaji hao waliookolewa wamepewa makazi, huduma za matibabu na chakula, na kufikishwa huko Dongola, mji mkuu wa Jimbo la Kaskazini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |