Shirika la habari la serikali ya Morocco limesema wahamiaji zaidi ya 400 kutoka nchi zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara jana Jumapili walijaribu kuvuka mpaka na kuingia kwenye eneo la Ceuta linalomilikiwa na Hispania. Baadhi ya wahamiaji hao na askari 24 walijeruhiwa kwenye tukio hilo. Polisi ya Morocco imewakabidhi wahamiaji hao kwa idara husika za nchi hiyo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |