Polisi nchini Tanzania wamewaua watu watatu wanaoshukiwa kuwa majambazi katika mji wa kibiashara nchini humo Dar es Salaam na kukamata silaha moja ikiwa na risasi.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam imesema, watuhumiwa hao waliuawa jumapili mchana katika eneo la Magomeni baada ya kurushiana risasi na polisi.
Taarifa hiyo imesema, uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa watuhumiwa hao wamefanya vitendo vya ujambazi jijini Dar es Salaam na mikoa mingine ya jirani kwa muda mrefu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |