Wataalamu wanasema endapo dunia inakabiliwa na changamoto mbalimbali za uchumi, baraza la uchumi duniani WEF la mwaka 2020 huko Davos litakuwa fursa nzuri kwa Afrika Kusini kuvutia uwekezaji.
Mchumi mkuu wa Investec Bw. Annabel Bishop amesema baraza hilo litatoa nafasi kwa ujumbe wa Afrika Kusini kueleza hali yake, na hatua gani zitakazotekelezwa au kupangwa kukabiliana na changamoto hizo.
Msemaji wa hazina ya taifa ya Afrika Kusini Ntsakisi Ramunasi amesema ujumbe wa Afrika Kusini utafanya mawasiliano kwenye jukwaa la WEF, wakati Afrika Kusini inakabiliwa na changamoto mbalimbali za ongezeko dogo la uchumi na shinikizo la kifedha, na kusema nchi hiyo itaendelea kufungua mlango kwa biashara na kuwa moja kati ya nchi zinazovutia uwekezaji zaidi duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |