Kocha Oliver Mbekela wa timu ya Cresta Cranes U-17 ya Uganda bado ana matumaini ya kufanya kazi nzuri katika mashindano yanayoendelea nchini Tanzania. Katika mechi iliyochezwa jumapili ya Kombe la Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 20 jijini Dar es Salaam, Tanzania iliifunga Uganda 2 – 1, lakini Uganda ilipata goli moja la ugenini, hivyo kuizuia Tanzania kuongeza fursa ya ushindi. Kocha huyo amesema wana matumaini kwa kuwa wana goli moja la ugenini, lakini kushindwa huko kumewapa fursa ya kujua ni maeneo gani wanapaswa kuyatilia maanani katika siku zijazo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |