Shirika la viwango Tanznaia (TBS) limeteketeza bidhaa za vyakula na vipodozi ambazo havikidhi viwango katika soko zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 10.
Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki, na kaimu mkuu wa Kanda ya kati, Salome Emmanuel, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye uteketezaji wa bidhaa hizo jijini Dodoma.
Bidhaa hizo zilikamatwa jijini Dodoma na Singida, kuanzia mwezi Oktoba hadi Desemba 2019. Aliwataka wafanyibiashara ambao wamekuwa na tabia hiyo ya kuuza bidhaa ambazo zimepitwa na muda wa matumizi, kuacha mara moja la sivyo wachukuliwe hatua kali za kisheria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |