Kamati ya haki za kibinadamu chini ya bunge la Iraq imesema, hivi karibuni maandamano yaliyofanyika huko Baghdad, mji mkuu wa nchi hiyo na sehemu nyingine yamesababisha vifo vya watu 10 na wengine 159 kujeruhiwa. Kamati hiyo imetoa taarifa ikizitaka pande mbalimbali kutotumia mabavu na kulinda mali za watu binafsi na umma. Tangu mwaka 2009 mwezi wa Oktoba, maandamano yametokea katika sehemu mbalimbali nchini humo kupinga ufisadi, upungufu wa huduma na ukosefu wa ajira.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |