Wadudu hao waharibifu walitua katika vijiji vya Kiambere na Mutuavale na inaaminika walitoka Kaunti ya Kitui.
Ripoti zilisema walivamia mashamba ya mawele na malisho na kusababisha uharibifu mkubwa.
Naibu kamishna wa Mbeere Kusini, Charles Igiha alisema waliingia Embu kupitia Isako karibu na mpaka wa kaunti hiyo na Kitui.
Bw Igiha alisema Wizara ya Kilimo imefahamishwa kuhusu uvamizi huo.
Kaunti nyingine zilizoathiriwa na wadudu hao ni Isiolo, Samburu, Wajir, Garissa, Marsabit, Laikipia, Mandera, Kitui, Baringo na Turkana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |