• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • TWCC yasema wanawake wengi wanashindwa kufanya biashara nje ya nchi kwa kutokuwa na elimu ya sheria

    (GMT+08:00) 2020-01-30 19:47:28
    Chama cha wafanyabiashara wnawake Tanzania (TWCC) kimesema kuwa wafanyabiashara wengi wanawake nchini humo wanashindwa kufanya biashara nje ya nchi kutokana na kutokuwa na elimu ya sheria pamoja na taratibu zinazotumika kwa biashara hizo.

    Maleko alisema kuwa hatua hiyo imekuwa ikiwazuia wanawake wengi kufanya biashara hizo, ukizingatia Tanzania imepata fursa ya uwapo wa soko la pamoja la Afrika Mashariki, lakini bado wanawake wengi hawajalitumia.

    Mwenyekiti huyo alisema kuwa kutokana na hali hiyo, chama hicho kiliandaa mkakati wa kuhakikisha kinazunguka nchi nzima na kukutana na wanawake wajasiriamali ili kuwapatia elimu ya ufanyaji biashara hiyo ambapo wamepanga hadi kufikia mwaka 2023 kuwafikia wanawake 10,000.

    Alisema mbali na kuwapatia elimu na mbinu za kufanya biashara hizo, chama hicho kimekuwa kikitumia fursa hiyo kuwapatia mikopo yenye riba nafuu kama mitaji pamoja na kuwaelimisha juu ya kutunza kumbukumbu za kifedha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako