• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakulima watakiwa kukata bima

    (GMT+08:00) 2020-01-31 19:42:38
    Wakulima katika mikoa ya Nyanda za juu Kusini wametakiwa kukata bima za kilimo kutoka kwenye kampuni ya Bima za kilimo ili kukabiliana na majanga mbalimbali yatokanayo na shughuli za Kilimo kwa lengo la kujihakikishia usalama wa mazao ya kilimo.

    Wito huo umetolewa jana na Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA) Kanda ya Nyanda za juu Kusini, Consolata Gabone.

    Alisema kwa sasa kuna mashirika mengi yanayotoa huduma za bima za kilimo katika mikoa ya nyanda za juu kusini na kuwa ni wakati mwafaka kwa wakulima hao kujiunga na Bima za Kilimo kwajili ya manufaa yao.

    Consolata alisema sekta ya kilimo imekuwa na mchango mkubwa sana kwajili ya maendeleo ya kilimo nchini na imekuwa ikichangia pato la taifa na hivyo ni muhimu kwa wakulima kujihakikishia usalama wa mazao yao kwa kukata bima za kilimo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako