Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Bw. Christopher Ngubiagai amesema, watu zaidi ya 13 wamefariki na wengine 15,096 wamepoteza makazi yako kutokana na mafuriko yaliyosomba vijiji 16 katika wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi, kusini mwa Tanzania.
Bw. Ngubiagai amesema, mvua kubwa inayoendelea kunyesha pia imeharibu maelfu ya ekari za mashamba na kuua mifugo.
Ameongeza kuwa mamlaka ya wilaya hiyo imetenga vituo vinne vinavyoweza kuwahifadhi watu elfu 8 waliopoteza makazi. Wengine 7,096 wanakaa kwenye nyumba za jamaa na marafiki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |