Rais Abdelmadjid Tebboune wa Algeria amesema Algeria na Tunisia zimekuwa na maoni ya pamoja kuhusu masuala ya kimataifa na kikanda, ukiwemo mgogoro wa Libya. Rais huyo amesema hayo katika mkutano na wanahabari na mwenzake wa Tunisia Kais Saied ambaye yuko ziarani nchini Algeria. Rais Tebboune pia ameahidi kuwa nchi yake itatoa dola milioni 150 za kimarekani kwa benki ya Tunisia kama mkopo, ili kuhimiza ukuaji wa uchumi wa nchi jirani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |