Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres na mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani WHO Bw. Tedros Ghebreyesus watahudhuria kikao cha 33 cha kawaida cha mkutano wa viongozi wa nchi na serikali za Umoja wa Afrika. Viongozi hao wawili watakuwa kati ya maofisa wa ngazi ya juu ambao watahudhuria mkutano huo utakaofanyika kuanzia Januari 21 hadi Februari 10 kwenye makao makuu huko Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |