Kaimu katibu mkuu mtendaji wa MTN Ali Monzer amesema kuna haja ya huduma za simu nchini Uganda kupanuliwa zaidi ikiwemo kufanya malipo mbali na kutuma na kupokea fedha. Ali amesema hiyo ndio njia pekee ya kuhakikisha Uganda inakumbatia uchumi wa kidigitali. Akizungumza Kampala Uganda, Ali amewataka wajasiriamali kusaidia juhudi hizo ikiwa ni mojawapo ya njia za kuuunda ajira kwa raia wengi nchini humo. Aneongeza kuwa nchi nyingi hivi sasa ikiwemo Kenya zimekuwa zikipanua huduma zao za simu kama vile ulipaji wa huduma na kusisitiza kuwa watu wengi nchini Kenya wamerahisisha mambo mengi kwa kutumioa simu.Ameongeza kuwa wajasiriamali ndio wenye ushawishi mkubwa zaidi na endapo watashirikiana na wengi basi uchumi wa kidijitali utafikiwa nchini Uganda.