Mwenyekiti wa baraza la utawala la Sudan Bw. Abdel Fattah al-Burhan amesema, mkutano wake na waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu ulikuwa ni kwa ajili ya malsahi ya taifa.
Bw. Burhan amesema mkutano huo ulilenga kuiondoa Sudan kutoka kwenye orodha ya Marekani ya nchi zinazounga mkono ugaidi. Jeshi la Sudan pia limeunga mkono mkutano huo na kusema umefanyika chini ya ufahamu wa waziri mkuu wa Sudan Bw. Abdalla Hamdok. Bw. Burhan alikutana na Bw. Netanyahu mjini Entebbe Uganda jumatatu iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |