• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yatenga shilingi bilioni 4 kwa ajili ya maendeleo ya kampuni za kilimo

    (GMT+08:00) 2020-02-06 09:51:56

    Kenya imetenga dola za kimarekani milioni 40 kwa ajili ya mfuko wa kampuni ndogo na zenye ukubwa wa kati SMEs ili kuhimiza ongezeko la uzalishaji wa kilimo nchini humo.

    Katibu mkuu tawala wa wizara ya maendeleo ya viwanda ya Kenya Bw. Lawrence Karanja, amesema mfuko huo utazipatia mikopo kampuni ndogo ambazo haziwezi kupata mikopo kutoka benki za biashara.

    Kwenye hafla ya usaini wa nyaraka kati ya wizara hiyo na idara 5 zitakazotoa mikopo, Bw. Karanja amesema serikali inatilia mkazo kustawisha kampuni ndogo na zenye ukubwa wa kati ambazo zinatoa nafasi nyingi zaidi za ajira nchini Kenya.

    Serikali pia itatoa mafunzo kwa viongozi wa kampuni ndogo ili kuinua uwezo wao wa usimamizi. Bw. Karanja amesema kampuni zisizopungua 400 zitanufaika. Ingawa Kenya ina benki nyingi, bado ni vigumu kwa kampuni ndogo kupata mikopo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako