• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya na Marekani zasaini mkataba wa kuruhusu usafirishaji wa moja kwa moja wa mizigo kwa ndege

    (GMT+08:00) 2020-02-06 19:52:44
    Kenya na Marekani zimetia saini marekebisho ya mkataba wa usafiri wa anga kati ya Marekani na Kenya,ambao utarahisisha uchukuzi wa bidhaa baina ya nchi hizo mbili.

    Marekebisho hayo,ambayo yameongeza haki zote za mizigo kwa mkataba uliopo wa usafiri wa anga,yanatarajiwa kurahisisha usafirishaji wa mizigo.

    Marekebisho hayo yameongeza uhuru wa anga kwa shughuli zote za mizigo,ikimaanisha gharama za chini na ufanisi katika usafirishaji mizigo.

    Katibu wa serikali ya Amerika anayeshughulika na uchumi na biashara,Manisha Singh na Waziri wa Uchukuzi wa Kenya James Macharia walitia saini mkataba huo alhamisi asubuhi jijini Washington,Marekani.

    Waziri Macharia alisema mktaba huo utawezesha upanuzi wa huduma za mizigo za ndege kwa kuruhusu mashirika mengi ya ndege kutoka nchi zote mbili kufungua na kuendesha vituo vya mizigo inayosafirishwa kwa ndege katika nchi zao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako