Msemaji wa polisi ya taifa ya Nigeria Frank Mba ametoa taarifa ikisema, wapiganaji wapatao 250 kutoka kundi lenye msimamo mkali wameuawa katika operesheni ya mapigano iliyofanywa na polisi katika jimbo la Kaduna, kaskazini kati mwa nchi hiyo. Wajumbe wa ngazi ya juu wa kundi la Ansaru lenye msimamo mkali ni kati ya waliouawa, wakati timu ya kikosi cha polisi iliyoungwa mkono na helikopta ikizindua operesheni dhidi ya kituo chao katika msitu wa Kuduru huko Kaduna.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |