Takwimu mpya zinazotolewa na idara ya takwimu ya Afrika Kusini zimeonesha kuwa kiwango cha ukosefu wa ajira cha Afrika hakikubadilika katika asilimia 29.1 kwenye robo ya nne ya mwaka jana. Ikilinganishwa na robo ya tatu ya mwaka jana, idadi ya watu walioajiriwa iliongezeka kwa elfu 45 na kufikia milioni 16.4, huku idadi ya watu wasio na ajira ikipungua kwa elfu 8 hadi milioni 6.7 katika robo ya nne ya mwaka jana ikilinganishwa na robo ya tatu ya mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |