Mshambuliaji wa timu ya Porto ambaye ni raia wa Mali, Moussa Marega, ametoka uwanjani kwa hasira baada ya kuitwa nyani katika mchezo mkali wa Ligi ya Ureno iliyochezwa kwenye uwanja hapo jana. Mchezaji huyo alifunga bao katika dakika ya 60 dhidi ya timu yake ya zamani, hivyo kuwafanya mashabiki wa timu hiyo ya nyumbani kuongeza chuki dhid yake. Dakika 71 ndani ya mchezo, Marega alitoa ishara kwa benchi la ufundi kuwa alikuwa anatoka nje ya uwanja kupinga ubaguzi huo, licha ya wachezaji wenzake, kocha wa Porto Sergio na wachezaji wa Vitoria, kumbembeleza asitoke uwanjani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |