Kili Canvas iliyozinduliwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro Lager hivi karibuni jijini Dar es Salaa,, imekuwa kivutio kikubwa kwa wakimbiaji wa jiji hilo. Canvas hiyo ina lengo la kuhamasisha wakimbiaji wa vitongoji vya jiji la Dar es Salaam na mji wa Moshi katika kuelekea kilele cha mbio za Kili Marathon zinazotarajiwa kufanyika Machi Mosi, mwaka huu mkoani Kilimanjaro. Meneja wa bia ya Kilimanjaro Lager, Pamela Kikuli amesema mtu yoyote anayependa mchezo wa kukimbia anaweza kupata fursa ya kupita katika canvas hiyo ya kisasa na kupigwa picha kisha kutumiwa katika simu yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |