Alisema, kitendo cha mwekezaji huyo mzawa kuwekeza nchini humo, ni manufaa kwa Taifa katika suala la kodi, ajira kwa Watanzania, lakini ni fursa kwa viwanda vingine kwani malighafi zinazotumika zinapatikana nchini humo.
Mbali ya kiwanda hicho, Waziri Bashungwa pia alitembelea kampuni ya wawekezaji wazawa ya GF Vehicle Assemblies kilichopo eneo la Tamco.
Kampuni hiyo inatarajia kuanza kuunganisha magari mchanganyiko yenye uzito usiozidi tani nane ambapo uzinduzi wake unatarajiwa kufanyika Mei mwaka huu.
Bashungwa aliwapongeza wawekezaji waliowekeza nchini, huku akitoa rai kwa mamlaka na taasisi zinazohusika na viwanda vidogo vidogo zikiwamo SIDO, DIT na NEMC kuwa karibu na wawekezaji kwa ushauri wa kitaalamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |