Siku chache baada ya Shirikisho la Soka Afrika CAF lipange makundi ya fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN), kocha wa timu ya taifa ya Uganda ya wachezaji wa ndani Johnathan Mckinstry ameeleza kuwa kwa sasa hofu yao ipo kwao wenyewe. Johnathan amesema kwa sasa ataandaa timu itakayojitoa kwa asilimia 100 kuelekea michuano ya CHAN itakayofanyika Cameroon kuanzia April 4-25 2020. Katika droo iliyochezeshwa Jumatatu hii, Uganda wamepangwa na timu za taifa za Togo, Morocco na Rwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |