Katibu Mkuu wa zamani wa shirikisho la soka Afrika CAF Amr Fahmy, 36, amefariki dunia baada ya kuugua ugonjwa wa saratani kwa miaka miwili. Amr kutoka nchini Misri alichaguliwa kuwa katibu mkuu wa CAF November 2017 kumrithi Hicham El Amrani lakini hakudumu hata kwa miaka miwili katika nafasi hiyo baada ya kuondolewa bila maelezo yoyote. Disemba mwaka jana Amr alitangaza kuwa na nia ya kugombea Urais wa shirikisho la soka Afrika (CAF) ifikapo mwaka 2021, na aliondoka CAF akiwa katika nafasi ya ukatibu mkuu baada ya kushindwa kuelewana na Rais wa CAF Ahmad Ahmad
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |