Emily Nakalema amekuwa mwanamke wa kwanza wa Uganda kushinda ngumi katika mchujo wa Fainali za Afrika zinazoendelea mjini Dakar, Senegal. Nakalema amepata ushindi huo kwa kumpiga Ivanusa Gomes Moreira, ambaye ni bingwa namba tatu wa Afrika katika uzito wa welterweight. Kwa sasa Nakalema amefikia ngazi ya nusu fainali, ikiwa ni nafasi ya juu zaidi kufikiwa na Mganda yoyote katika kuwania tiketi ya kushiriki mashindano ya Olimpiki ya Tokyo yatakayofanyika baadaye mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |