Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) Dk. Devota Marwa amesema alikosea kuwania uongozi ndani ya taasisi hiyo. Dk. Marwa amesema ameshindwa kutimiza ndoto yake licha ya kudumu madarakani kwa miaka mitatu, na katika muda huo, amekuwa akitumia fedha zake za mfukoni kwa kazi za chama, hivyo hatagombea tena katika uchaguzi wa mwezi Desemba mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |