Takwimu zilizotolewa na Shirikisho la viwanda la China zinaonyesha kuwa, asilimia 97.08 ya uzalishaji umerejeshwa katika viwanda 500 vikubwa vya utengenezaji nchini China.
Takwimu hizo zilipatikana baada ya kufanya uchunguzi kuhusu data za viwanda 491 kati ya Februari 18 na 20, ambao haukuhusisha viwanda 9 vilivyopo Hubei, mkoa ulioathiriwa vibaya na maambukizi ya virusi vya korona.
Hivi sasa mashirika ya sekta mbalimbali nchini China yanafanya juhudi kusaidia viwanda kurejesha uzalishaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |