Jeshi la Uturuki limeanza operesheni za kijeshi za "ngao ya spring" dhidi ya jeshi la serikali ya Syria mkoani Idilib, Syria, ili kulipiza kisasi dhidi ya shambulizi lililosababisha vifo na majeruhi kwa askari wengi wa Uturuki. Kwa mujibu wa wizara ya ulinzi wa taifa ya Uturuki, operesheni hizo zinalenga kujilinda na kuangamiza jeshi la serikali ya Syria mkoani humo. Hadi sasa, operesheni hizo zimewaua wanajeshi 1,212 wa jeshi la serikali ya Syria, na kuharibu ndege moja isiyo na rubani, helikopta 8 na vifaru 103.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |