Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) Harambee Starlets ya Kenya walitangaza ushiriki wao katika mashindano ya kimataifa ya Turkish Women's Cup kwa kishindo baada ya kuilipua Northern Ireland Under-19 kwa mabao 2-0 mjini Alanya, Uturuki, Jumatano usiku. Warembo wa kocha David Ouma, ambao wamealikwa kushiriki mashindano hayo ya tatu kwa mara yao ya kwanza, wanashikilia nafasi ya pili katika Kundi B kwa tofauti ya ubora wa magoli na Chile walioifunga Black Queens kutoka Ghana 3-0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |