Uongozi wa Yanga na mdhamini GSM wamehaidi kutoa Sh milioni 200 kwa wachezaji wa Yanga iwapo watashinda mechi yao dhidi ya Simba Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa. Afisa Mhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema wadhamini wa GSM wameweka mezani Sh Milioni 200 kwa wachezaji endapo watapata ushindi wa aina yoyote siku hiyo. Naye kocha, Luc Eymael amesemaa amewasoma Simba kwa muda mrefu tangu alipowasili nchini Tanzania kukinoa kikosi hicho na amegundua mambo mengi ya kuwadhibiti wapinzani wao. Amesema atashambulia mwanzo mwisho kwa kasi, tofauti na michezo iliyopita kwani, Boniface Mkwasa, kocha Msaidizi wa Yanga amemweleza vitu vingi kuhusu mchezo huo
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |