Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na LaLiga ya Hispania wameandaa kongamano la michezo ambalo litawashirikisha viongozi wa Shirikisho hiko na klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara. Mkurugenzi wa Masoko wa TFF Boniface Wambura amesema, katika kongamano hilo la siku tatu, washiriki watapata elimu ya utendaji wa shughuli za maendeleo ya soka. Mwakilishi wa LaLiga, Alvaro Paya amesema kongamano hilo litagusa mambo mbalimbali ikiwemo utendaji, masoko na jinsi ya kuziwezesha klabu nchini Tanzania kujikwamua na kujiendesha kisasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |