• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Uchukuzi wa mizigo kwa SGR waleta shilingi bilioni 7.5

    (GMT+08:00) 2020-03-06 20:09:19
    Ripoti ya Shirika la Takwimu nchini Kenya KEBS inaonesha kuwa uchukuzi wa mizigo kutumia reli mpya (SGR) ililetea nchi mapato ya shilingi bilioni 7.54 ikibeba tani 3.25 za mizigo kwa kipindi cha miezi tisa kufikia Septemba 2019.

    Hata hivyo, ripoti hiyo imeonyesha kuwa upande wa uchukuzi wa mizigo uliimarika huku idadi ya watu wanaosafiri kupitia treni ikipungua kwa watu 200, 000.

    Idadi ya abiria wanaotumia SGR ilipungua kutoka milioni 1.38 kwa kipindi kama hicho mwaka wa 2018 hadi 1.18 milioni mwaka jana.

    Hii inaashiria kuwa sheria kali zilizowekwa katika saa za kuabiri treni na ushindani kutoka kwa kampuni za mabasi na ndege zinazolipisha bei nafuu zimewafanya abiria wengi kuacha kutumia SGR.

    Kulingana na KNBS mapato ya shilingi bilioni 4.09 ya biashara ya kubeba mizigo na SGR kwa miezi hiyo tisa ya mwaka jana, ilikuwa mara mbili ya mwaka wa 2018.

    Wafanyabiashara walianza kulipa Sh51, 275 kwa kasha la futi 20 na Sh70,000 kwa kasha la futi 40 ambayo ni mara mbili ya bei ya mvuto ya Sh25,000 hadi Sh35,000.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako