Mkurugenzi mtendaji wa miradi ya dharura ya afya wa WHO Michael Ryan amesema, kwa sasa hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa maambukizi ya COVID-19 yatatoweka katika majira ya joto, pia amezitaka nchi mbalimbali zipambane na virusi hiyo kwa sasa.
Kwenye taarifa ya kila siku, Bw. Michael amesema bado tabia ya virusi katika mazingira tofauti ya hali ya hewa haijulikana, na kuonya tarajio kwamba virusi vitatoweka vyenyewe katika majira ya joto.
Ameongeza kuwa tunapaswa kudhania kuwa maambukizi ya virusi hivyo yataendelea kuwa na uwezo wa kuenea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |