Askari wawili wameuawa katika mlipuko mkubwa uliotokea katika mkoa wa Chlef ulioko umbali wa kilomita 200 magharibi mwa Algiers. Wizara ya ulinzi ya Algeria imetoa taarifa ikisema, mlipuko huo ulitokea wakati jeshi hilo likifukua bomu lililotengenezwa kienyeji. Taarifa hiyo imesisitiza kuwa jeshi hilo litaendelea na juhudi kuwasaka wahalifu waliosalia na kuwaangamiza popote walipo kote nchini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |