Wizara ya afya ya serikali ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imekanusha uvumi kwamba maambukizi ya COVID-19 yamegunduliwa nchini humo. Wizara hiyo imetoa taarifa ikisema, habari hizo zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari na channeli za televisheni kuhusu kugunduliwa na kuthibitishwa kwa maambukizi ya COVID-19 nchini humo si za kweli.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |