Real Madrid imepata kichapo cha kushtukiza cha bao 2 – 1 kutoka kwa Real Betis wakiwa ugenini, kichapo kilichoiporomosha Real Madrid hadi nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi, ikiwa nyuma kwa point mbili dhidi ya mahasimu wao Barcelona. Hivi sasa Real Madrid ina point 56 huku Barcelona wakishika uongozi wa Ligi hiyo baada ya kuinyuka Real Sociedad bao 1 – 0. Nahodha wa Real Madrid Sergio Ramos amesema wamekubali kupoteza mchezo huo, ingawa walijipanga kupata matokeo mazuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |