Wanariadha nyota nchini Tanzania akiwemo Alphonce Simbu wamethibitisha kushiriki Sokoine Marathon 2020 itakayofanyika April 11 jijini Arusha. Mbio hizo ambazo hufanyika kila mwaka ni mahsusi kwa ajili ya kumuenzi aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine, aliyefariki dunia April 12, 1984. Mratibu wa mbio hizo. Wilhelm Gidabuday amesema, Simbu pamoja na wanariadha wengine wamethibitisha kushiriki mbio hizo ambazo maandalizi yake yameanza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |