Uongozi wa Azam FC umesema sababu ya kuwaongezea mikataba ya miaka mitatu nyota wao watatu ni kuendeleza vipaji vyao na pia kutimiza maombi ya benchi la ufundi la timu hiyo. Walioongezewa mikataba ni mabeki Lusajo Mwaikenda na Oscar Masai, pamoja na mshambuliaji Andrew Simchimba. Nyota hao watakuwa na timu hiyo kwa miaka mitatu zaidi kila mmoja, hivyo kuwa katika dimba la Chamazi hadi mwaka 2023.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |