Baada ya kupoteza mechi tatu mfululizo ugenini, Kocha Mkuu wa Aliiance FC, Felix Minziro amesema kucheza mechi mfululizo ni chanzo vha matokeo hayo mabaya. Jumamosi, Alliance ilifungwa 1 – 0 na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ikiwa ni baada ya kufungwa na Yanga na Ruvu Shooting. Minziro amesema hawezi kuwalaumu wachezaji wake kupoteza mchezo huo kutokana na ukweli kuwa wamejituma ili kupata matokeo mazuri lakini bahati haikuwa kwao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |