Waziri mkuu wa Sudan Abdallah Hamdok amenusurika katika jaribio lililoshindwa la kumuua katika mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum.
Kituo cha taifa cha televisheni nchini humo hakikutoa taarifa zaidi kuhusu jaribio hilo. Hata hivyo, mashuhuda wa tukio hilo wamesema, msafara wa Hamdok ulishambuliwa kwa bomu lililotegwa kwenye gari katika mlango wa kuingilia kwenye kambi ya jeshi la nchi hiyo mjini Khartoum.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |