Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amelaani vikali mauaji ya mfanyakazi wa kiraia wa Tume ya kulinda amani ya Umoja huo nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR.
Bw. Guterres ametoa salamu za rambirambi kwa familia ya mhanga aliyeuawa Jumamosi mjini Ndele, na pia ametoa wito kwa mamlaka za Afrika ya Kati kufanya juhudi kuwatambua na kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wa mauaji hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |