• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ethiopia yachukua hatua kukabiliana na mlipuko wa COVID-19

    (GMT+08:00) 2020-03-10 09:36:43

    Kamati ya kitaifa ya mawaziri ya kukabiliana na maambukizi ya COVID-19 nchini Ethiopia, imetangaza hatua mbalimbali za kuzuia mlipuko wa COVID-19 nchini humo.

    Kamati hiyo iliyoundwa wiki iliyopita kwa ajili ya kufuatilia kwa karibu juhudi zinazoendelea za kuzuia mlipuko wa COVID-19 nchini humo, imemwarifu Waziri Mkuu wa Ethiopia Bw. Abiy Ahmed kuhusu juhudi zinazoendelea za kuitayarisha nchi hiyo dhidi ya maambukizi ya COVID-19.

    Kwa mujibu wa kamati hiyo, kwa kushirikiana na mashirika mengine husika, wizara ya afya ya Ethiopia imeanzisha kituo cha dharura cha saa 24 cha kukabiliana na maambukizi ya COVID-19, wakati huo huo, upimaji kwa wasafiri wote wanaoingia nchini kupitia ardhi na anga pia unaendelea.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako