Tammy Abraham amekataa ofa ya kusaini mkataba mpya na klabu yake ya Chelsea. Mshambuliaji huyo alicheza kwa mkopo Aston Villa msimu wa 2018 -19 katika Ligi Daraja la Kwanza na kuisaidia timu hiyo kupanda daraja msimu huu kabla ya kurejea Stamford Bridge, ambako amejihakikishia nafasi kama mshambuliaji chaguo la kwanza. Hivi karibuni, Chelsea walimpa ofa ya mkataba mpya, lakini mchezaji huyo amekataa na kutaka alipwe pesa ndefu kama anayolipwa Callum Hudson-Odoi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |