Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amelaani vikali shambulizi dhidi ya msafara wa waziri mkuu wa Sudan Bw. Abdalla Hamdok.
Bw. Guterres amesema ni lazima kuhakikisha kuwa watu waliofanya shambulizi hilo wanafikishwa mbele ya sheria, na kusisitiza kuwa Umoja huo unaunga mkono juhudi za amani nchini Sudan.
Bw. Hamdok alinusurika baada ya msafara wake kushambuliwa mapema jana kwa bomu lililotegwa kwenye gari mjini Khartoum.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |